WATENDAJI ARDHI WATAKIWA KUTOCHELEWESHA HUDUMA KWA MAKUSUDI

    Na  Munir Shemweta, WANMM IRINGA   Serikali imewataka watendaji wa sekta ya Ardhi nchini kutochelewesha huduma za sekta ya Ardhi kwa mak...

Latest Post

WATENDAJI ARDHI WATAKIWA KUTOCHELEWESHA HUDUMA KWA MAKUSUDI

Written By CCMdijitali on Saturday, February 1, 2025 | February 01, 2025

  

Na Munir Shemweta, WANMM IRINGA

 

Serikali imewataka watendaji wa sekta ya Ardhi nchini kutochelewesha huduma za sekta ya Ardhi kwa makusudi wakati wanapowahudumia wananchi wanaokwenda kupata huduma katika ofisi zao.

 

Hayo yameelezwa Januari 31, 2025 mkoani Iringa na Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani wa Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Bw. Hamdouny Mansoor wakati wa kikao kazi cha watumishi wa sekta ya Ardhi Mkoa wa Iringa.

 

Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Mhandisi Anthony Sanga, Bw. Mansoor amesema kumekuwa na ucheleweshaji huduma kwa makusudi na wakati mwingine watendaji wa sekta ya Ardhi kuwatuma mwananchi wanaokwenda kupata huduma.

 

"Sasa anakuja mwananchi anasema anataka kulipa kodi anaelezwa, aah hiyo kazi ni ya Afisa Ardhi nenda kulee mimi mpima,  si umuelekeze tu, wakati mwingine tunatoa kauli ambazo siyo nzuri kwa wananchi wanaofika kupata huduma za Ardhi kwenye ofisi zetu" amesema.

 

Aidha, Mansoor kupitia kikao hicho kilichoandaliwa na Ofisi ya Kamishna wa Ardhi Msaidizi Mkoa wa Iringa ametaka kuwekwa utaratibu rasmi katika ofisi zote za Ardhi kuanzia ngazi ya wilaya wa namna ya kupata hati ili wananchi wauelewe na  kuufuata utaratibu huo.

 

"Inasisitizwa ili upate hati ni vitu gani vya msingi vinatakiwa viwepo kwa wananchi kupata hati yake, viainishwe na vibandikwe katika ofisi zetu za ardhi" amesema.

 

Kwa upande wake  Kamishna wa Ardhi Msaidizi Mkoa wa Iringa Bw. Frank Minzikuntwe ameeleza kuwa, kikao kilichofanyika cha watumishi  kilikuwa na lengo la  kuzungumza na kupeana mikakati pamoja na mipango kazi ya namna ya kushughulikia kero na utoaji huduma za sekta ya ardhi kwa haraka zaidi.

 

"Sisi kama watendaji wa sekta ya Ardhi katika mkoa wa Iringa tunaahidi watumishi wote katika ngazi ya mkoa tutafanya kazi kwa weledi na uaminifu na kuwahudumia wananchi kwa tija ili waweze kupata huduma kwa wakati unaostahili’’. amesema

 

Kikao hicho cha siku moja kimeshirikisha watendaji wa sekta ya ardhi kutoka halmashauri zote za mkoa wa Iringa pamoja na wale wa Ofisi ya Kamishna wa Ardhi Msaidizi mkoa wa Iringa.


Sehemu ya watumishi wa sekta ya ardhi mkoa wa Iringa wakifuatilia majadiliano wakati wa kikao kazi cha watumishi wote wa sekta ya ardhi mkoa wa Iringa kilichofanyika jana.

Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Bw. Hamdouny Mansoor akizingumza wakati wa kikao kazi cha watumishi wa sekta ya ardhi mkoa wa Iringa kilichofanyika jana mkoani humo.

Kamishna wa Ardhi Msaidizi mkoa wa Iringa Bw. Frank Minzikuntwe akizungumza katika kikao kazi cha watumishi wa sekta ya ardhi mkoa wa Iringa jana. (PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI)

Sehemu ya watumishi wa sekta ya ardhi mkoa wa Iringa wakifuatilia majadiliano wakati wa kikao kazi cha watumishi wote wa sekta ya ardhi mkoa wa Iringa kilichofanyika jana.




THBUB YATEMBELEA VYUO VYA MAFUNZO YA AMALI, PEMBA

 THBUB YATEMBELEA VYUO VYA MAFUNZO YA AMALI, PEMBA


TUME ya Haki za Binaadamu na Utawala Bora (THBUB) imefanya ziara ya kuvitembelea vyuo

viwili vya Mafunzo ya Amali vya Vitongoji, Wilaya ya Chake Mkoa wa Kusini Pemba na cha

Daya Mtambwe, Wilaya ya Wete, Mkoa wa Kaskazini Pemba, kwa lengo la kutoa elimu na

kujenga uelewa mpana kwa jamii juu ya dhana nzima ya Haki za Binadamu na Misingi ya

Utawala Bora.


Maafisa wa Tume hiyo, Ofisi ya Pemba wakiongozwa na Afisa Uchunguzi Ndg. Ramadhani Slaa

wameifunza jamii juu ya umuhimu wa kutambua Haki za Binaadamu na Utawala Bora pamoja

ushiriki na kuanzisha klabu za Haki za Binaadamu katika vyuo na kuwashauri wanafunzi wa vyuo

hivyo kujiunga na klabu hizo.


Akizungumza kwenye ziara hiyo, ofisi za chuo cha Vitongoji, Bw. Slaa alieleza nia ya ziara yao

chuoni hapo mbali na kutoa elimu ya Haki za Binaadamu na Utawala Bora lakini kushirikiana na

vyuo hivyo kuanzisha Klabu za Haki za Binadamu na Utawala Bora ili kukuza ushirikiano na nguvu

ya pamoja kwa kuongeza uelewa kwa jamii juu dhana ya Haki za Binaadamu na misingi ya Utawala

Bora.


Aidha, Bw. Ramadhan Slaa awasihi wanafunzi vyuoni humo kuendelea kuwa mabalozi wazuri wa

jamii zao katika kueneza dhana halisi ya Haki za Binaadamu na misingi ya Utawala Bora ili kukuza

jamii yenye uelewa mpana kwa maeneo hayo.


Katika hatua nyengine, THBUB ilimshauri, Mkuu wa chuo cha Daya cha Mtambwe, Mwl. Saada Ali

Hamad, kuanzisha Klabu ya Haki za Binadamu na Utawala Bora chuoni hapo ili kuongeza hamasa

na uelewa zaidi kwa jamii.


Naye, Mwalimu dhamana wa Chuo cha Mafunzo ya Amali cha Vitongoji na Mkuu wa Idara ya

Masomo Mtambukwa chuoni hapo, Mwl. Khamis Abdalla Khamis alitoa shukrani kwa THBUB kwa

kuwatembelea chuoni hapo sambamba na kuishauri Tume kuwa karibu na Klabu hizo ili kuzijengea

uimara na ziwe endelevu pamoja na kuahidi kuzisimamia vyema katika kuendeleza shughuli za

kutoa elimu kupitia klabu hizo.


Halikadhalika,kwa nyakati tofauti wanafunzi wa vyuo viwili hivyo, walipata nafasi ya kuuliza maswali

kuhusu dhana na uelewa wa Haki za Binaadamu na Utawala Bora pia kutaka kujua umuhimu na

faida za kujiunga na Klabu za Haki za Binadamu na Utawala Bora vyuoni humo.


Kwaupande mwengine, wanafunzi hao wameiomba THBUB kurudi tena kwenye vyuo vyao na

kujenga utamaduni wa kuwatembelea mara kwa mara ili wajifunze zaidi. Hata hivyo, waliiahidi Tume

kuongeza ushiriki wao mpana katika kusimamia na kuendeleza klabu hizo ndani ya vyuo vyao.


Kiasi cha wanafunzi wasiopungua 600 wakiwemo 400 kutoka Chuo Cha mafunzo ya Amali cha

Vitongoji na 200 kutoka chuo cha Daya, Mtambile kwa nyakati tofauti walihudhuria hafla hiyo

iliyowajenga kitaaluma na kuelezwa juu ya umuhimu wa kushiriki klabu kama hizo na umuhimu wake

wa kuanzishwa kwenye vyuo vyao.

MAOFISA kutoka Tume ya Haki za Binaadamu na Utawala Bora (THBUB) wakiwapa elimu ya uelewa mapana juu ya dhana ya Haki za binaadamu na misingi ya Utawala Bora katika vyuo vya Mafunzo ya Amali vya Vitongoji na Daya, Pemba.



WANAFUNZI wa Chuo Cha Mafunzo ya Amali wa chuo cha Daya, mtambile,Wilaya ya Wete, Mkoa wa Kaskazini Pemba wakiwasikiliza Maofisa kutoka Tume ya Haki za Binaadamu na Utawala Bora (THBUB) juu ya uelewa mpana wa dhana ya Haki za binaadamu na misingi ya Utawala Bora.


WANAFUNZI wa Chuo Cha Mafunzo ya Amali wa chuo cha Daya, mtambile,Wilaya ya Wete, Mkoa wa Kaskazini Pemba wakiwasikiliza Maofisa kutoka Tume ya Haki za Binaadamu na Utawala Bora (THBUB) juu ya uelewa mpana wa dhana ya Haki za binaadamu na misingi ya Utawala Bora.


MAOFISA kutoka Tume ya Haki za Binaadamu na Utawala Bora (THBUB) wakiwapa elimu ya uelewa mapana juu ya dhana ya Haki za binaadamu na misingi ya Utawala Bora katika vyuo vya Mafunzo ya Amali vya Vitongoji na Daya, Pemba.



MWISHO.

 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link