Asema Rais Dkt. Samia ametoa shilingi bilioni 130 kwa ajili ya ukarabati madaraja mkoa wa Lindi. Awatoa hofu wakazi na watumiaji wa barabara ya Dar, Lindi. WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amet ...

Read more »

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema Serikali ya Awamu ya Sita itaendelea kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini ikiwemo kuimarisha hali ya u ...

Read more »

 Na Mwandishi wetu, ArushaMamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA) imeendelea na zoezi la kuwajengea uwezo wazabuni kuhusu matumizi ya Moduli ya kuwasilisha na kushughulikia malalamiko na rufa ...

Read more »

 Kaimu Naibu Wakili Mkuu wa Serikali, Bi. Vivin Method akizungumza na watumishi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali wakati akifungua Mafunzo kuhusu Upimaji wa Afya yaliyofanyika jijini Dar es Sa ...

Read more »

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Ukraine zimekubaliana kuongeza ushirikiano katika sekta mbalimbali za kiuchumi na kijamii ikiwemo kilimo, biashara na uwekezaji, viwanda, utalii, elimu n ...

Read more »

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb), amewasili jijini Antalya, Uturiki kwa ziara ya kikazi anayotarajia kuifanya nchini humo kuanzia Aprili ...

Read more »

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt, Hussein Ali Mwinyi ameeleza kuwa Ziara yake Uingereza imekuwa na Manufaa Makubwa kwa Zanzibar kwani Wawekezaji wengi wameonesha dhamira ya k ...

Read more »

Na Mwandishi WetuMAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Stephen Wasira amesema Chama cha Demokrasia na Maendeleo hakina hoja ya msingi ya kuzuia Uchaguzi Mkuu mwaka huu kwani kama ni mabadilik ...

Read more »

MAJALIWA AIPA MAAGIZO TANROADS UKARABATI WA BARABARA NA MADARAJA

Asema Rais Dkt. Samia ametoa shilingi bilioni 130 kwa ajili ya ukarabati madaraja mkoa wa Lindi.   Awatoa hofu wakazi na watumiaji wa baraba...

Latest Post

WAZIRI KOMBO ATEMBELEA UBALOZI WA TANZANIA NCHINI MALAWI, AAZIMIA KUIMARISHA USHIRIKIANO.

Written By CCMdijitali on Friday, February 28, 2025 | February 28, 2025

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Mahmoud Thabit Kombo, amefanya ziara rasmi katika Ubalozi wa Tanzania jijini Lilongwe, Malawi, kwa lengo la kukagua miundombinu ya ubalozi huo, kupokea taarifa za maendeleo, na kusikiliza changamoto zinazokabili shughuli za kidiplomasia.

 

Katika ziara hiyo, Mhe. Kombo alikutana na Balozi wa Tanzania nchini Malawi, Mhe. Agnes Kayola, pamoja na maafisa wa ubalozi, ambapo alipokea taarifa kuhusu hali ya mahusiano ya kidiplomasia, uchumi, siasa, na usalama kati ya Tanzania na Malawi.

 

Taarifa hiyo ilihusisha pia masuala ya mali za Serikali ya Tanzania zilizopo nchini Malawi, ustawi wa watumishi wa ubalozi, na mchango wa Watanzania waishio Malawi katika maendeleo ya taifa.

 

Aidha, Waziri Kombo alipokea maelezo kuhusu fursa mbalimbali zinazoweza kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi kati ya mataifa hayo mawili, hususan katika uwekezaji, biashara za mpakani, na sekta ya utalii.

 

Akizungumza na maafisa wa ubalozi, Mhe. Waziri alisisitiza umuhimu wa kuitangaza vyema Tanzania kimataifa na kutumia fursa zilizopo kwa manufaa ya maendeleo ya taifa. Alitoa wito kwa Watanzania waishio Malawi kushirikiana na ubalozi katika kukuza uhusiano wa kidiplomasia, kiuchumi, na kijamii kati ya nchi hizo mbili.

 

Kwa upande wake, Balozi Agnes Kayola alimshukuru Waziri Kombo kwa ziara yake na kuahidi kuwa ubalozi utaendelea kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi kwa maslahi ya Tanzania.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Mahmoud Thabit Kombo akisoma kitabu cha taarifa cha Ubalozi alichopewa na Balozi wa Tanzania nchini Malawi.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Mahmoud Thabit Kombo (katikati) akiwa na  Balozi wa Tanzania nchini Malawi Mhe. Agnes Kayola (kushoto) na kulia ni Mkuu wa Utawala David Fupi.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akisaini kitabu cha wageni kwenye makazi ya Balozi wa Tanzania nchini Malawi.



SERIKALI KUENDELEA KUBORESHA UWEKEZAJI NA UKUAJI WA UCHUMI

 Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), amesema kuwa Serikali inaendelea kuboresha mazingira ya uwekezaji na ukuaji wa uchumi nchini.

Dkt. Nchemba alisema hayo jijini Dodoma wakati akifungua Mkutano wa Majadiliano ya Kimkakati kati ya Serikali na Washirika wa Maendeleo Ngazi ya Juu, ambao unalenga kubadilishana maarifa, taarifa, na uzoefu kuhusu sera na mikakati ya maendeleo ya nchi.

Alisema Serikali imewasilisha bungeni Muswada wa Sheria ya Uwekezaji Tanzania (Tanzania Investment Act, 2024) na kuanzisha Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi (Tanzania Investment and Special Economic Zones Authority) ili kuboresha mazingira ya uwekezaji. 

“Serikali kupitia Chemba ya Biashara, Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA) na Kituo cha Uwekezaji kati ya Sekta Binafsi na Umma (CPPP) imeendeleza majadiliano kati ya sekta ya umma na sekta binafsi ili kuongeza ushiriki wa sekta binafsi katika maamuzi”, aliongeza Mhe. Dkt. Nchemba.

Mhe. Dkt. Nchemba ambaye ni Mwenyekiti wa Mkutano huo, alisema Serikali pia inaandaa Mkakati wa Kitaifa wa Uendelezaji wa Uwekezaji (2025/2026 – 2034/2035) ambao utakuwa na mpango wa utekelezaji, ufuatiliaji na tathmini, unaoeleza majukumu ya kila mdau na viashiria vya kupima maendeleo.

Dkt. Nchemba alibanisha kuwa katika kipindi cha mwezi Julai 2024 hadi Desemba 2024, Serikali imeongeza uwezo wa uzalishaji umeme kwa asilimia 30.3, hasa kupitia Mradi wa Umeme wa Maji wa Julius Nyerere (JNHPP) ili kupunguza gharama za biashara.

“Kupitia Sheria ya Fedha ya mwaka 2024, Serikali imepunguza au kuondoa ada na tozo mbalimbali ili kuboresha mazingira ya biashara”, aliongeza Mhe. Nchemba.

Dkt. Nchemba alisema Serikali pia imepata mafaniko makubwa katika ukuaji wa uchumi jumuishi ambapo idadi ya shule na wanafunzi imeongezeka, vituo vya afya vimeongezeka na huduma zimeboreshwa, huduma za maji zimeongezeka katika maeneo yote nchini pamoja na ongezeko la ajira.

Aidha, alitoa rai kwa wadau wote kushirikiana kwa karibu na Serikali ili kufanikisha utekelezaji wa Mwongozo wa Ushirikiano wa Maendeleo (DCF) ambao umetilia mkazo utaratibu wa ufadhili wa miradi ya mabadiliko ya tabianchi (climate financing modality) na kuimarisha Ushirikiano kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP) kama njia mbadala za ufadhili.

Kwa upande wake Mwenyekiti Mwenza wa Kundi la Washirika wa Maendeleo na Balozi wa Ireland nchini, Mhe. Nicola Brennan aliishauri Serikali kuendelea kuboresha mazingira ya biashara kwa kuondoa vikwazo vinavyozuia uwekezaji wa moja kwa moja wa kigeni.

Alisema hii itaongeza mchango wa sekta binafsi katika kuleta uwekezaji, ajira, uvumbuzi, na suluhisho kwa changamoto mbalimbali ili kujenga uchumi imara.

“Wadau wa Maendeleo tayari tumekuwa na majadiliano mazuri kuhusu hili, na tunapongeza utayari wa Serikali kushirikiana nasi kuona jinsi bora ya kuondoa vikwazo na kuvutia uwekezaji zaidi wa moja kwa moja wa kigeni (FDI) nchini Tanzania, pamoja na kuimarisha sekta ya biashara ya ndani”, aliongeza.

Mhe. Brennan alisema Washirika wa Maendeleo watahakikisha kuwa Dira ya Maendeleo ya Mwaka 2050 inapata ufadhili wa uhakika na endelevu, hasa katika sekta za afya, elimu na sekta ya kijamii kwa ujumla.

“Tunapopanga vipaumbele katika matumizi ya rasilimali finyu za Msaada wa Maendeleo (ODA), ni muhimu pia kuelewa vyema vyanzo vingine vya ufadhili vinavyopatikana kwa nchi zenye kipato cha kati nje ya ODA, pamoja na mchango ambao sisi kama Wadau wa Maendeleo tunaweza kutoa kusaidia Tanzania kuzifikia na kuzitumia fursa hizo ipasavyo. Tunatazamia kujadili zaidi suala hili kwa kina.”

Aliahidi kuwa Washirika hao wataendelea kushirikiana na Tanzania kuhakikisha maendeleo yanapatikana na kustawisha jamii.



















Mhe. Dkt. Philip Mpango amewasili Jijini Windhoek nchini Namibia

Written By CCMdijitali on Thursday, February 27, 2025 | February 27, 2025

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango leo tarehe 27 Februari 2025 amewasili Jijini Windhoek nchini Namibia ambapo anatarajia kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Maombolezo ya Kitaifa na Ibada ya kumuaga aliyekuwa Rais wa kwanza wa Jamhuri ya Namibia hayati Dkt. Sam Nujoma.

Utoaji wa heshima za mwisho na Ibada ya kumuaga Kitaifa hayati Dkt. Nujoma itafanyika katika Uwanja wa Michezo wa Uhuru uliopo Jijini Windhoek tarehe 28 Februari 2025 na Mazishi yatafanyika katika eneo la Makaburi ya Mashujaa yaliyopo katika Jiji la Windhoek nchini Namibia tarehe 01 Machi 2025.


Published from Blogger Prime Android App


Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App

TANZANIA NA MALAWI ZASAINI HATI YA MAKUBALIANO KATIKA AFYA NA MKATABA WA KUHAMISHA WAFUNGWA

Written By CCMdijitali on Wednesday, February 26, 2025 | February 26, 2025

 Tanzania na Malawi zimesaini hati ya makubaliano katika sekta ya afya na mkataba wa kuhamisha wafungwa , ikiwa ni hatua muhimu ya kuendelea kuimarisha ushirikiano kati ya mataifa haya mawili jirani.

Makubaliano hayo yamesainiwa tarehe 26 Februari 2025 wakati wa Mkutano wa Sita wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano (JPCC) kati ya Tanzania na Malawi uliofanyika jijini Lilongwe, Malawi.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.) aliyeongoza ujumbe wa Tanzania alisaini makubaliano hayo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Malawi Mhe. Nancy Tembo alisaini pia makubaliano hayo.

Akizungumza katika mkutano huo, Waziri Kombo amesema kusainiwa kwa makubaliano haya ni moja ya mafanikio ya mkutano huo na ni hatua muhimu katika kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Malawi.

Mhe. Waziri amezihimiza taasisi na sekta husika kuhakikisha makubaliano hayo yanatekelezwa kwa tija na ufanisi ili kuleta manufaa kwa wananchi wa pande zote mbili.

Kwa upande wake, Waziri wa Mambo ya Nje wa Malawi, Mhe. Nancy Tembo, amepongeza hatua hiyo muhimu na kubainisha kuwa kusainiwa kwa makubaliano hayo ni chachu ya mabadiliko katika sekta za afya na haki za wafungwa.

Ameeleza kuwa ushirikiano huo utaimarisha huduma za afya na kusaidia katika kusimamia haki za wafungwa walioko katika magereza ya mataifa hayo.

Mbali na kusainiwa kwa makubaliano hayo, mkutano huo pia umejadili maeneo mengine ya ushirikiano kati ya Tanzania na Malawi, yakiwemo biashara, elimu, miundombinu, nishati, na usalama wa mipaka.

Viongozi wa pande zote mbili wameahidi kuhakikisha kuwa uhusiano wa kirafiki kati ya mataifa hayo unaendelezwa kwa manufaa ya wananchi wao.

Pia, wamekubaliana kuwa utekelezaji wa makubaliano hayo unapaswa kufanyika kwa wakati ili kuhakikisha kuwa malengo yaliyokusudiwa yanafikiwa  na kuongeza ushirikiano wa pande mbili kwa kiwango cha juu zaidi.

Mkutano huo wa JPCC ulitanguliwa na kikao cha Maafisa Waandamizi kutoka Tanzania na Malawi uliofanyika tarehe 25 Februari 2025.







TAASISI ZA UMMA NA SEKTA BINAFSI SHIRIKIANENI -WAZIRI KOMBO

 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Mahmoud Thabit Kombo, amezitaka taasisi za umma na sekta binafsi kushirikiana kwa karibu na kuchangamkia fursa mbalimbali za maendeleo kwa lengo la kukuza uchumi na kuhakikisha maendeleo endelevu.

Akizungumza na ujumbe wa Tanzania unaoshiriki Mkutano wa Sita wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (JPCC) kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Malawi, Waziri Kombo alisisitiza kuwa mshikamano wa wadau wa sekta zote ni nguzo muhimu katika kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

"Maendeleo endelevu hayawezi kupatikana bila mshikamano thabiti kati ya taasisi zetu. Ushirikiano wa karibu, mbinu bunifu, na matumizi sahihi ya fursa zilizopo ni nyenzo muhimu kwa mafanikio ya pamoja," alisema Waziri Kombo.

Aidha, alihimiza washiriki wa mkutano huo kutumia majukwaa kama JPCC kuimarisha ushirikiano wa sekta mbalimbali ili kufanikisha utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo inayolenga kuinua uchumi wa mataifa yote mawili.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaib Mussa, alisisitiza umuhimu wa taasisi za umma kushirikiana kwa karibu kupitia vikao kama ili kubaini maeneo mapya ya ushirikiano, kutatua changamoto kwa pamoja, na kuboresha utekelezaji wa miradi iliyopo.

"Ni muhimu kushirikiana kwa karibu, hasa tunapokuwa kwenye majukwaa kama haya, ili kutatua changamoto zinazotukabili kwa pamoja na kufanikisha malengo ya maendeleo," alisema Balozi Mussa.

Ujumbe wa Tanzania katika mkutano huo umejumuisha viongozi na maafisa kutoka taasisi za umma, ikiwemo Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

Wengine ni Wizara ya Nishati, Wizara ya Miundombinu, Mawasiliano na Usafirishaji ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Wizara ya Uchukuzi, Wizara ya Ulinzi na Usalama, Wizara ya Viwanda na Biashara, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Shirika la Viwango Tanzania (TBS), na Idara ya Uhamiaji.

Mkutano huu wa JPCC unalenga kujadili na kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Malawi katika sekta mbalimbali, ikiwa ni pamoja na biashara, uwekezaji, nishati, afya, ulinzi na usalama, miundombinu, usafirishaji, na ulinzi.






ZIARA YA RAIS SAMIA BUMBULI, LUSHOTO MKOANI TANGA

Written By CCMdijitali on Monday, February 24, 2025 | February 24, 2025

 RAIS MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AENDELEA NA ZIARA YAKE  YA KIKAZI BUMBULI,LUSHOTO MKOANI TANGA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi wa Bumbuli, wilayani Lushoto katika muendelezo wa ziara yake mkoani Tanga  24 Feb, 2025



 

RAIS MWINYI: TUSIPANDISHE BEI ZA BIDHAA ZA VYAKULA WAKATI WA RAMADHANI

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Hussein Ali Mwinyi ameeleza kuridhishwa na upatikanaji wa Bidhaa za Vyakula na kuwataka Wafanyabiashara Kutopandisha Bei wakati Ramadhani itakapoanza.


Rais Dkt.Mwinyi amesema hayo alipotembelea Masoko ya Jumbi , Mwanakwerekwe na Darajani kuangalia Mwenendo wa Biashara na Upatikanaji wa Bidhaa za Vyakula kuelekea Mwezi Wa Ramadhani.

Aidha Rais Dkt.Mwinyi ameeleza kuwa Serikali inajipanga kwa ajili ya Ujenzi wa Masoko mengine maeneo mbalimbali ili kila Mfanyabiashara afanye biashara kwenye mazingira rasmi .

Kuhusu Suala la Usafi wa Masoko ameuagiza Uongozi wa Masoko hayo kutafuta njia Bora zaidi ya Uhifadhi wa Bidhaa za Wafanyabiashara ili Masoko kuwa safi wakati Wote.

Amezielekeza Taasisi zinazosimamia Masoko hayo kuhakikisha Upatikanaji wa Huduma ya Maji na Vipooza hewa katika Masoko yote pamoja na kuimarisha Usafi.

Ziara hiyo ya Rais Dkt, Mwinyi ni ya Kwanza tangu kufunguliwa kwa Masoko Mapya ya Jumbi , Mwanakwerekwe na Ukarabati Mkubwa wa Soko la Darajani.










TAMISEMI YAKUSUDIA KUBORESHA ZAIDI HUDUMA ZA MACHO SEKTA YA AFYA YA MSINGI

Written By CCMdijitali on Thursday, February 20, 2025 | February 20, 2025

 OR-TAMISEMI


Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa – TAMISEMI, imesema itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali katika kuimarisha upatikanaji wa huduma za macho katika sekta ya afya ya msingi, kwa kuhakikisha miongozo na sera zinazoongoza utoaji wa huduma hizo zinaendelea kuboreshwa kwa manufaa ya wananchi.

Hayo yameelezwa leo Februari 20, 2025 jijini Dodoma na katibu Mkuu OR – TAMISEMI Adolf Ndunguru kupitia hotuba yake iliyosomwa na Mkurugenzi wa Idara ya Afya,Ustawi wa jamii,na Lishe Dkt. Rashidi Mfaume katika hafla ya uzinduzi wa mpango wa macho imara, utakaotekelezwa katika mikoa minne ya Arusha, Singida, Tabora na Manyara.

Dkt. Mfaume amesema kutokana na  eneo la afya ya macho kupewa kipaumbele cha chini, OR – TAMISEMI kwa kushirikiana na wizara ya Afya, na wadau mbalimbali imejipanga kuhakikisha huduma za macho zinajumuishwa katika mfumo wa afya ya msingi ili kuwafikia watoto wengi zaidi katika jamii.

Naye, Mkurugenzi wa huduma za uuguzi na ukunga Dkt. Ziada Sellah akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama, amesema inakadiriwa kuwa wastani wa watoto nane kati ya kila watoto 10,000 wenye umri wa miaka 0 -15, wana ulemavu wa kutokuona na idadi kubwa zaidi wana upungufu wa kuona. 

“Serikali itaendelea kuboresha huduma za Uzazi, Mama na Mtoto ikiwemo za uchunguzi wa macho na kutoa afua sahihi kwa watoto tangu wakiwa tumboni mwa mama zao hadi wanapofika umri wa miaka mitano, kipindi hiki ni muhimu sana kwani ndio matatizo mengi yasababishayo ulemavu wa kutokuona hutokea,” amesema Dkt. Sellah

Awali, akitoa taarifa ya mpango huo, Daktari Bingwa wa macho kutoka Chuo cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili, Prof. Milka Mafwiri amesema lengo la mpango huo ni kupunguza ulemavu wa kutokuona  unaozuilika kwa Watoto hapa nchini kwa kujumuisha afua za afya ya macho kwa watoto katika afya ya msingi hususani kwenye huduma za afya ya uzazi, mama na mtoto.

Kwa mujibu wa Prof. Mafwiri mpango huo unaogharimu Sh.Bilioni 4.9 na utatekelezwa kwa muda wa miaka mitano katika halmashauri 16 za mikoa ya Arusha, Singida, Tabor ana Manyara.

Mpango huo uliopewa kaulimbiu ya uoni bora, Maisha bora, unakuja wakati ambao watoto milioni 1.4 duniani, wanakabiliwa na tatizo la kutoona huku nusu ya idadi hiyo wakiwa ni Watoto wanaoishi katika nchi zinazoendelea ikiwamo Tanzania.






RAIS MWINYI: SMZ ITAENDELEA KUWEKA MAZINGIRA WEZESHI KWENYE BIMA.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt,Hussein Ali Mwinyi ameeleza kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa Kushirikiana  na Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) Itaendelea kuweka Mazingira  Wezeshi kwenye soko la Bima ili kuongeza Pato la Taifa kupitia Sekta hiyo.

Rais Dkt.Mwinyi ameyasema hayo alipopokea  Taarifa ya Soko la Bima kwa Mwaka 2023  iliofanyika  Hoteli ya Verde , Wilaya ya Mjini, Mkoa wa Mjini Magharibi. 

Aidha Rais Dkt.Mwinyi amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Zina dhamira ya dhati ya kuleta Maendeleo kwa Wananchi kutokana na Mageuzi makubwa yanayoendelea  kufanyika katika sekta zote za Kiuchumi.

Amefahamisha kuwa ili Mageuzi hayo yafanikiwe ni vema Sekta ya Bima iendane na Kasi ya Serikali zote mbili kwa kujikita kwenye Ubunifu na Matumizi ya Teknolojia na Watoa Huduma za Bima na Wadau wote wafanye kazi kwa Weledi na Ushirikiano.

Halikadhalika Rais Dkt.Mwinyi amesisitiza kuongezwa jitihada zaidi katika Matumizi ya Tehama, Ubunifu wa bidhaa za Bima na utoaji wa Elimu ya Bima kwa Wananchi.

Vilevile  Rais Dkt.Mwinyi amebainisha kufanyika kwa Utafiti wa aina ya Vihatarishi vinavyotakiwa kupewa kinga  kupitia Bima kwa Mali za Serikali na Mamlaka ya Bima   Ipitie Sheria na Kanuni mbalimbali za Bima ili ziendane na Mazingira  ya sasa na Ukuaji wa Uchumi.

Kwa upande mwingine Rais Dkt.Mwinyi amewasisitiza Wananchi na Wadau kuendelea kutumia huduma za Bima  na Mamlaka husika zifanye bidii ya kuhakikisha  Nchi inanufaika na Huduma hizo.

Ameipongeza Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania kwa Kuanzisha Ofisi ya TIRA kanda ya Unguja na Ofisi ya Kanda ya Pemba na kusisitiza Kutolewa Elimu zaidi kwa Wananchi ili wapate Uelewa zaidi wa Masuala ya Bima.



















1234567 Next

SPORTS

 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link